Tuesday, July 21, 2015

PICHAZ: HAWA NDIO MASTAA WAKUBWA WA NIGERIA WALIOFUNGA NDOA ZA KIFAHARI DUNIAN 2015

 JAPOKUWA mwaka huu wa 2015 umepita nusu yake ni mengi yametokea katika ulimwengu wa burudani ambapo waburudishaji  wengi walioanza mwaka wakiwa ‘wapweke’ hivi sasa wana wenza wao waliofunga nao ndoa na wanategemea kufanya hivyo kabla mwaka huu haujaisha.
 Mtandao wa Nigeriafilms.com umekuwa ukiweka kumbukumbu na sasa unaweza kuonyesha ndoa za ‘nguvu’ ambazo zimetamba katika nusu ya kwanza ya mwaka 2015. 
Paul Okoye na AnitaIsama . 
Ndoa ya kimila iliwakutanisha Peter, mmoja wa mapacha wa kundi la muziki la Psquare alipomchukua mpenzi wake wa siku nyingi na mama wa mtoto wake, , Anita Isama. Tukio hilo lilifanyika mwezi Januari huko Ikoyi, Nigeria
Peter Okoye na Lola Omotayo-Okoye.
Kama ilivyokuwa kwa kaka yake, mwanamuzaiki  maarufu,  Peter Okoye, na mama wa watoto wake wawili, Lola Omotayo, waliimarisha uhusiano wao kwa kufunga ndoa huko Ikoyi.
Chris Attoh na  Damilola Adegbite.
Wawili hawa walioana siku ya Wapendanao ya Valentine -- Februari 14 – katika ndoa ya kimyakimpya jijini Accra, Ghana ambapo biharusi Damilola Adegbite alikutana na mpenzi wake, mtoto wa mfalme wa kikabila huko Ghana, Chris Attoh, kwenye mahojiano ya kipindi cha televisheni cha Mnet cha Tinsel.
Japokuwa wawili hao wanasema watafunga ndoa nchini Nigeria,  marafiki zao wanasema wana hamu ya kuona hilo linatokea kabla ya kumalizika kwa mwaka 2015.
Gbenro Ajibade na  Osas Ighodaro.
NI dhahiri Gbenro Ajibade bado ana furaha isiyomithilika kwa kumuoa kipenzi chake, Osas Ighodaro, ambaye hadi sasa bado wako kwenye fungate.  Wawili hao walioana Jumamosi ya Julai 4, 2015 jijini New York Marekani.:

No comments:

Post a Comment